Posts

Showing posts from 2017

KIFAHAMU CHAKULA CHA KUZUIA KUZEEKA HARAKA

Image
Maisha ya sasa hivi yamegubikwa na matumizi ya vipodozi vya kuzuia uzee hadi kufikia kiwango cha kuonekana kama ni chakula kuliko vitu vya urembo. Vipodozi hivyo huja kama creams, visafisha ngozi au serums. Lakini ieleweke kuwa kutumia vipodozi vya kuondoa uzee juu ya ngozi hakuwezi kuwa mbadala wa chakula ambacho kinaboresha mwonekano na kutunza ngozi yako kuanzia ndani. Chakula cha kuzuia kuzeeka haraka ndiyo kitu muhimu katika kuufanya mwili wako usizeeke haraka na katika kuulinda mwili wako kutokana na mionzi ya UV (ultra violet) ambayo ndio chanzo kikuu cha mistari na mikunyanzi juu ya ngozi yako. Ungana nami leo kuona ni chakula gani kinasaidia kutunza mwonekano wako wa ujana.  Lakini kwanza tuvichambue vitu muhimu katika  chakula vyenye uwezo wa kulinda mwili wako usizeeke haraka. Vitu Muhimu Katika Chakula Vya Kuzuia Kuzeeka Haraka Katika mada yetu ya  Ondoa Uzee  tuliona kwamba mahitaji ya mwili hubadilika kadri umri unavyosonga mbele na kwamba ili kudumisha

MKANDA WA JESHI NI NINI?

Image
Mkanda wa jeshi (shingles) ni jina linalotumika mitaani kuutaja ugonjwa unaoshambulia ngozi na kujenga tabaka la vijipele vikubwa venye majimaji ambavyo mara nyingi hukamata upande mmoja wa mwili. Ingawa vijipele vya mkanda wa jeshi vinaweza kutokea sehemu yo yote ya mwili, mara nyingi hupenda kuota kifuani, shingoni, usoni, mgongoni na mikononi. Vijipele hivi hukaa juu ya ngozi kwa muda wa wastani wa wiki mbili hadi sita kisha hupotea. Vipele vya mkanda wa jeshi huambatana na maumivu makali na kusikia ngozi kuwaka moto. Aghalab ugonjwa huu humrudia mtu zaidi ya mara moja. Mkanda wa jeshi huwapata zaidi watu wenye umri mkubwa, zaidi ya miaka 50, utafiti ukionyesha kuwa zaidi ya nusu ya watu wenye umri wa zaidi ya miaka 80 hupatwa na mkanda wa jeshi. Vilevile huwapata zaidi watu waliopatwa na magonjwa yanayopunguza kinga za mwili, kama vile,  UKIMWI  na  saratani . Tiba za mionzi na chemotherapy huweza kupunguza kinga za mwili za mgonjwa na kumfanya awe kwenye hatari kubwa y

IFAHAMU HOMA YA INI – HEPATITIS B

Image
Mada yetu ya leo ni mfululizo wa mada iliyopita iliyoelezea ugonjwa wa homa ya ini (hepatitis). Katika ukurasa uliopita tuliona kuwa hepatitis ni jumla ya magonjwa yote yanayoshambulia seli za ini. Tuliona kuwa kuna aina kuu tano ya hepatitis ingawa katika ukurasa huo tulizungumzia kwa undani aina moja tu – hepatitis A. Katika ukurasa huu basi tutaendelea kuona aina nyingine ya hepatitis yaani hepatitis B. Hepatitis B ni maambukizi mabaya sana ya kirusi aitwaye hepatitis B virus (HBV) kwenye maini. Kwa watu wengine ugonjwa huu huweza kuchukua zaidi ya miezi 6 (chronic). Ugonjwa huu ukichukua muda mrefu unaweza kuleta madhara ya kufeli kwa ini, kansa ya ini au liver cirrhosis hali ambayo itaacha makovu ya kudumu kwenye maini. Watu wengi wanaougua ugonjwa huu hupona kabisa. Kuna chanjo ya kusaidia kuzuia hepatitis B lakini hakuna tiba pale ambapo tayari utakuwa umeambukizwa virusi wa hepatitis B. Ukishaambukizwa yafaa kuchukua tahadhari za kusaidia kutowaambukiza watu wengine

HITIMISHO ....Tiba Ya Kisukari Kwa Kutumia Insulin Pump

Image
TIBA YA KISUKARI KWA KUTUMIA INSULIN Tumekwisha kuona ni  chakula gani apate mgonjwa wa kisukari  na kwa mpango upi mgonjwa wa kisukari apate chakula hicho. Pia tulijadili jinsi ya kufanya mazoezi ya mwili na kuona faida za mazoezi hayo kwa mgonjwa huyu. Katika mada yetu ya leo, tutazungumzuia namna ambavyo mgonjwa wa kisukari anavyoweza kupewa au kutumia insulin. Kimsingi mgonjwa anaweza kupewa insulin ya vidonge, lakini pindi atakapokunywa vidonge hivyo na vikafika tumboni, vitameng’enywa mara moja bila hata kuingia katika mkondo wa damu. Hivyo basi inapasa kumpa mgonjwa insulin ya sindano ambayo itachonmwa kwenye mafuta yaliyo chini tu ya ngozi, ili taratibu dawa hiyo iingie kwenye mkondo wa damu. Kuna aina zaidi ya 20 za insulin ambazo kila kila moja inafanya kazi tofauti na nyingine, imetengenezwa kwa njia tofauti na nyingine na ina bei tofauti na nyingine. Insulin nyingi hutengenezwa kwenye maabara na nyingine hutokana na wanyama, hasa nguruwe. Tiba Ya Kisukari

MUENDELEZO WA SOMO NA ZIJUE TIBA ZA KISUKARI: CHAKULA NA MAZOEZI KWA MGONJWA WA KISUKARI

Image
TIBA ZA KISUKARI: CHAKULA NA MAZOEZI KWA MGONJWA WA KISUKARI Hapo zamani, kabla ya uvumbuzi wa insulin (1921), ugonjwa wa kisukari, Type 1 Diabetes, ulikuwa ni ugonjwa ulioua watu wengi sana miaka michache tu baada ya mtu kuupata ugonjwa huo. Lakini sasa mambo yamebadilika kwa kiasi kikubwa sana. Mtu mwenye ugonjwa huu anaweza kuishi maisha ya kawaida kabisa, ili mradi anakuwa na mpango mzuri wa chakula, mazoezi ya kutosha na anatumia insulin. Kuwa mgonjwa wa kisukari maaana yake ni kukubali namna ya kuishi na siyo kushindwa kufanya jambo lo lote lile ulilokusudia. Unaweza kufanya biashara zako, kushiriki michezo na kufikia malengo yako bila tatizo lo lote. Kuna orodha ya watu wengi waliokutwa na kisukari na wakafanya vizuri katika michezo, siasa, uigizaji wa filamu, muziki, uandishi wa habari n.k. Kinachotakiwa ni kuwa na mpango mzuri wa kula, mazoezi ya kutosha na kuzingatia tiba unayopewa na daktari wako. Hakuna sababu KAMWE ya kushindwa kufikia malengo yako. Mfano mzuri ni

JE !!!! UNAZIFAHAMU DALILI NA MADHARA YA UGONJWA WA KISUKARI TAZAMA HAPA NA S.O.G

Image
DALILI NA MADHARA YA KISUKARI Tuliona katika ukurasa mwingine kuwa kisukari ni ugonjwa ambao humsababishia mtu kuwa na kiwango kikubwa cha sukari katika damu na kushindwa kuitumia sukari hiyo ipasavyo ili kumpa nguvu na hivyo sukari hiyo kutoka nje ya mwili wa mgonjwa kupitia njia ya mkojo. Ugonjwa huu pia huitwa Diabetes Mellitus, maneno yanayotokana na kigiriki na kilatini. Diabetes linatokana na kigiriki likimaanisha kijibomba kinachonyonya maji na mellitus linatokana na neno la kilatini “Mel” lenye maana ya asali, hivyo diabetes mellitus ni “kunyonya maji yenye utamu kama asali” baada ya madaktari wa enzi hizo kugundua kuwa mkojo na damu ya mgonjwa wa kisukari vilikuwa na glucose kwa wingi sana. Wachina wa zamani nao waligundua kuwa mchwa walijaa kwa kwingi kwenye eneo la mkojo wa mtu mwenye kisukari kutokana na mkojo huo kuwa mtamu na wakatoa neno “Sweet Urine Disease” -Ugonjwa wa kutoa mkojo mtamu. Insulin Na Kongosho Insulin ni homoni inayotoa ishara kwa seli

UFAHAMU UGONJWA WA KISUKARI NA HATARI ZAKE

Image
KISUKARI, UNAJUA CHANZO NA TIBA YAKE? Kisukari ni kundi la magonjwa yanayohusiana na ufanyaji kazi wa mwili ambapo mtu anakuwa na kiwango kikubwa cha sukari aina ya glucose katika mwili kutokana na  mwili wake kukosa uwezo wa kutengeneza insulin ya kutosha au seli za mwili wake haziwezi kutumia insulin iliyopo au pengine mwili kuwa na matatizo yote mawili kwa pamoja. Mgonjwa wa kisukari hupata haja ndogo mara kwa mara (polyuria), kusikia kiu kila wakati (polydipsia) na njaa (polyphagia). Kuna aina tatu za kisukari; Type 1 Diabetes, Type 2 Diabetes na Gestational Diabetes. 1. Type 1 Diabetes Mwili wa mgonjwa wa aina hii ya kisukari hautengenezi insulin kabisa. Kisukari cha aina hii mara nyingine huitwa insulin-dependent diabetes, juvenile diabetes, au early-onset diabetes. Watu huwa na kisukari aina hii wanapokuwa na umri wa chini ya miaka 40 na hasa katika miaka ya mwanzo kabisa ya ujana wao. Kisukari cha aina hii huwapata watu wachache ukilinganisha na aina nyingi