Timua Timua CCM, Hongera M/Kiti Magufuli, Wapinzani Mjifunze Kutoka CCM...!!!!!
Mimi ni miongoni mwa watu ninaotatizwa sana na ukiukwaji wa haki
unaofanyika popote ndani ya JMT na ni miongoni mwa watu wa mwanzo mwanzo
kabisa kumuita rais wetu Dr.John Pombe Magufuli kuwa ni dikiteta.
Katika tumbua tumbua majipu ya rais Magufuli niliunga mkono dhana nzima
ya utumbuaji na dhima ya utumbuaji ila sikuunga mkono utekelezaji wa
utumbuaji huo kutokana na baadhi ya utumbuaji kufanywa kidikiteta kwa
chuki, papara na double standards za hali ya juu kwa kukiuka sheria,
taratibu na kanuni.
Lakini kwa hii timua timua ya kuwatimua vigogo wa CCM, nimefarijika sana
kwa sababu kumbe huu utumbuaji wa kidikiteta sio kwa serikali tuu bali
hata kwa CCM. Hii ni plus kwa Magufuli kuwa katika tumbua tumbua,
anatumbua tuu bila kumuangalia mtu usoni kuwa nani ni nani, kama mtu
kama Sofia Simba ameweza kutumbuliwa, then kiukweli Magufuli sio mchezo!
.
Hakuna ubishi kuwa CCM ni chama kikongwe kinafanya mambo yake kiutu
uzima. Kwenye katiba yake kinazo taratibu za nidhamu zilizofuatwa ndani
kwa ndani, kimya kimya hadi kufikia hatua ya mwisho ya watu kupigwa
chini ndipo umma unaambiwa na kupigwa na surprise. Huu ni ukomavu na
ndiko kufanya maamuzi makubwa kiutu uzima. Pongezi ziende kwa Mwenyekiti
Magufuli. Wapinzani mjifunze kutoka CCM.
Ugomvi wa Baba na Mama.
Mara nyingi watoto huwa hawawezi kufahamua kuwa kumbe baba na mama huwa
wanagombana mara mara ugomvi wa kimya kimya chumbani. Mara kwa mara
wanawake huwa wanachukia na kuwanyima 'chakula' waume zao, hivyo kuna
wanaume kibao hulala njaa na hawasemi. Kuna wanawake kibao hubakwa na
waume zao na wengine hupokea hadi vipigo lakini hawasemi. Kuna mara
kibao baba na mama wamenuniana ila akija mgeni warajikausha.
Ugomvi ukiwa mkubwa hadi mama kufungasha ndipo hakuna namna lazima watoto watajua. Hiki ndicho kilichofanyika CCM.
Watuhumiwa wote walijadiliwa toka vikao vya chini kimya kimya. Wakapewa
barua za mashitaka yao, wakapewa muda wa kujibu tuhuma, wakaitwa
kujieleza, wakahojiwa na kupewa muda wa haki ya kusikilizwa na
kujitetea, kisha vikao vikafikia maamuzi kimya kimya na hatimaye ndipo
vikao vya maamuzi vikatangaza maamuzi yale. Huu ni ukomavu wa hali ya
juu na CCM kinastahili pongezi za dhati kwa hili.
Siku Polepole akiongea na media, awahakikishie Watanzania kuwa taratibu
zilifuatwa vinginevyo kama ule udikiteta wa kukanyaga katiba ya nchi pia
umeikanyaga katiba ya CCM hivyo timua timua ile ni muendelezo wa
udikiteta ule ule, CCM kitakuwa ni chama cha kidikiteta na kama
kinaongozwa kidikiteta na kiongozi dikiteta, then jiulize taifa letu la
Tanzania tunalipeleka wapi? .
Chedema utumieni uzoefu na ukongwe wa CCM katika kufanya maamuzi yake
kwa kuzingatia katiba zenu, niliwahi kuwashauri hivi kuhusu udikiteta
katika kuendesha mambo yenu ya ndani.
Fanyeni mambo yenu kimya kimya, jifunzeni kwa CCM ili angalau 2020
Watanzania tuweze kuwafikiria tuwajaribishe vinginevyo tutaendelea
kiongozwa na chama kikongwe kilichozeeka mpaka basi lakini kila
kinapofanya face lift kama hii, kinarudia ujana hivyo hata hapo mlipo
kama mnajidhania mmesimama, angalieni msianguke come 2020.
Hongera sana CCM kwa mabadiliko. Hongera kwa ukomavu.
Jumatatu njema
Comments
Post a Comment