Nimejaribu kujiua zaidi ya mara nne- Saida Karoli



Saida Karoli ambaye aliwahi kufanya vizuri na nyimbo kama ‘Mapenzi kizunguzungu’, Kaisiki, Maria Salome na nyingine kibao na alifanikiwa kuliteka soko la Afrika Mashariki kwa nyimbo hizo na kujipatia umaarufu mkubwa mwanzoni mwa miaka ya 2000, amefunguka kuwa amewahi kujaribu kuataka kujiua.

Akizungumza katika Promo ya mahojiano ya kipindi cha #TakeOne kinachorushwa na CloudsTv Saida karoli amesikika akisema kuwa ameshawahi kufanya majaribio ya kutaka kujiua zaidi ya mara nne.


Hata hivyo kupitia Promo hiyo amesikika akisema akisema yeye ni Mama wa watoto watano ambapo kila mtoto ana baba yake na kongeza kuwa hana mpango kutoa kizazi hivyo ataendelea kuzaa mpaka Mungu atakapowambia basi.

Comments

Popular posts from this blog

Picha ya kutisha ya Mtoto wa miezi nane kulawitiwa na baba yake mzazi.

MAJANI YA MPERA NA FAIDA ZAKE MWILINI.